Tuesday, October 25, 2016

Ajichinja kwa wivu wa Mapenzi






Ajichinja kwa wivu wa Mapenzi
Na Antony Sollo Mpwapwa.

Mtu mmoja amenusurika kifo katika stendi ya mabasi Wilayani Mpwapwa baada ya kujichinja kwa kutumia kitu chenye ncha kali kwa kile kilichodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Tukio hilo limetokea Oktoba 25 majira ya saa 7: 53 mchana katika stendi ya mabasi Wilayani Mpwapwa, mtu huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja alichukua uamzi huo baada ya kukataliwa na mwanamke aliyedaiwa kuwa alikuwa ni mpenzi wake.

Chanzo cha taarifa kutoka Wilayani Mpwapwa zimeeleza kuwa kijana huyo ni mgeni katika maeneo hayo na kwamba alikuja kumfuatilia mpenzi wake akitokea Mkoani Iringa ambapo baada ya kufika katika maeneo hayo,alikuta mpenzi wake akiwa na mwanamme mwingine jambo lililosababisha kuchukua uamzi wa kujitoa roho

Hata hivyo juhudi za kujitoa uhai kwa kijana huyo ziligonga mwamba baada ya Askari wa Jeshi la Polisi kufika katika eneo la tukio kumchukua na kumkimbiza  hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa kwa matibabu.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi kuzungumzia tukio hilo simu yake iliita bila majibu na juhudi za kumtafuta zinaendelea ili kuweza kuthibitisha taarifa  hizo

Sunday, October 23, 2016

TANGAZO KWA WANAUME WOTE TANZANIA


Wadau wa Chanma cha kutetea Haki za wanaume Tanzania napenda kuwataarifu kuwa tunarudi kuwaletea matukio mbalimbali ya ukiukwaji wa Haki za Wanaume Nchini Tanzania na Duniani kote.
Karibuni saaana!