Sunday, July 16, 2017

Barua ya Wazi kwa Waziri wa Fedha.





Mh Waziri,
Naomba kuwasilisha Malalamiko yangu kwako kuhusu vitendo nilivyofanyiwa na
kampuni ya Tujijenge Microfinance iliyoko katika mtaa wa New Bagamoyo Rd. Plot 17, Block 45A yenye Makao yake Makuu jijini Dar es salaam Dar Es salaam

 Mimi ni mwananchi mkazi wa jiji la Dar es salaam, niliomba Mkopo wa Shilingi milioni arobaini (40,000,000/) kwa ajili ya kuimarisha biashara yangu tangu 25 March mwaka huu na kutimiza masharti ikiwemo kufanyiwa tathmini ya biashara yangu  hivyo kukubaliwa kupatiwa fedha nilizoomba lakini hadi sasa niko njiapanda sijui la kufanya japokuwa kwa mujibu wa mashharti ya Kampuni hiyo  nilitakiwa niwe nimepatiwa mkopo huo ndani ya siku saba baada ya kukamilisha masharti ya mkopo huo.

Mh Waziri nimesikitishwa na watendaji wa Shirika hilo baada ya kuniingiza katika mgogoro mkubwa kutokana na kuchukua mkopo katika taasisi  ndogo za fedha baada ya kuhakikishiwa kuwa nimefuzu kupatiwa mkopo huo ndani ya siku saba lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea.

Nilikuwa na mpango wa kukuza biashara yangu kwa kununua basi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi ,nimesumbuliwa sana,nimetumia zaidi ya shilingi milioni mbili kwa ajili ya mawasiliano usafiri paomja na muda na kuingia madeni yaliyopelekea kuchukuliwa vitu vyangu nilivyoweka kama dhamana .kutokana na ahadi niliyokuwa nimetoa kwa wateja wangu kwamba ningekamilisha suala hilo kwa muda lakini hadi sasa  sijui kinachoendelea.

Kufuatia hali hii nimeingia gharama kubwa  yakiwemo madeni kutokana na ahadi za watendaji wa Kampuni hii zinazofikia mil 2 pamoja na kuchukuliwa kwa mali zangu zenye thamani zaidi ya shilingi milioni nane ambapo jumla ya madai yote ni shilingi milioni kumi( 10,000,000 ) na ninaomba uingilie kati mgogoro huu kufuatia baadhi ya  taasisisi za fedha kuendesha shughuli zao bila kuzingatia Sheria za Nchi.
Nimejitahidi kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huu bila mafanikio sasa naomba msaada maana mpaka sasa nimeingia katika matatizo makubwa ikiwemo kuyumba kwa uchumi na mahitaji ya familia maana nimetumia fedha nyingi katika ufuatiliaji ikiwemo kuweka mafuta kwenye magari ya maafisa wa Shirika hilo kwa nyakati tofauti hasa baada ya kuhakikishiwa kuwa nimefuzu kupata mkopo lakini hadi sasa nimetelekezwa.

Kwa barua hii naiomba Serikali iingilie kati suala hili ili haki iweze kutendeka.

BARAKA BEATUS MASHAURI
                                       S L P
                                       DAR ES SALAAM