Monday, April 15, 2013

KITWANGA ACHARUKA SAKATA LA KIWANDA CHA SAYONA KUNYANYASA WAFANYAKAZI



KITWANGA ACHARUKA SAKATA LA KIWANDA CHA SAYONA KUNYANYASA WAFANYAKAZI.
Na Antony Sollo  -Mwanza.
15 April 2013
Mbunge wajimbo la Misungwi ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Charles Kitwanga ‘Mawe Matatu”amesema kuwa iwapo manyanyaso wanayopata wafanyakazi na wananchi walioko katika kiwanda cha Sayona kilichopo eneo la Nyang’homango kata ya Usagara Jijini Mwanza hayatakomeshwa na vyombo vinavyohusika ataiacha Ofisi yake kwenda kushughulika na suala hilo mpaka kieleweke.
 
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akizungumza na Mwanaharakati wa Haki za Binadamu aliyetembelea Kiwanda cha Sayona na kujionea jinsi wananchi pamoja na wafanyakazi wa kiwanda hicho wanavyonyanyaswa na mwekezaji wakiwanda hicho.
Kitwanga alisema kuwa amesikitishwa  na taarifa iliyotolewa kwake na mwanaharakati huyo ambapo taarifa hiyo ikionyesha mapungufu makubwa yaliyopo katika kiwanda cha Sayona hususani katika kulinda maslahi ya wafanyakazi ikiwemo ukiukwaji wa Haki za binadamu na ukiukwaji wa Sheriaya Fidia kwa Wafanyakazi (Workmens’ Compensation Ordinance), Cap.263 ya 1948.
Sheria hii ilitungwa ilikutoa fidia kwa wafanyakazi wanaopata ajali au maradhi yanayotokana nakazi. Sheria hii pia inakwenda sambamba na sheria ya kutaarifua Ajari na maradhi yatokanayo na kazi ambayo iliitwa “Accidents and Occupational Diseases” (Notification) Ordinance, Cap 330.

Mwaka1953 marekebisho yalifanyika katika sheria hiyo (Sura 263) kwa
Kutungasheria nyingine Na. 25 ya1953 ambayo ilikuwa na lengo la
Kumlazimisha mwajiri kutoa taarifa kwa Afisa Kazi wa eneo husika
Pale mfanyakazi anapoumia au kupata ugonjwa unaotokanana
kazi.
Taarifa hiyo pia ilionyesha mambo mengi ikiwemo kutotolewa kwa taarifa kwa uwazi kuhusu matukio yanayotokea kiwandani hapo ikiwemo milipuko inayotokea na jinsi wahanga wa milipuko hiyo wanavyohudumiwa na haki zao kuhusu kuumia pamoja na vifo vinavyotokea ikiwamo na fidia wanazopaswa kulipwa wahanga na familia za wafanyakazi waliokufa wakiwa kazini.

Imegundulika kuwa Wafanyakazi wa kiwanda cha Sayona  kuwa hufukuzwa bila kufuatwa kwa kanuni na taratibu kwa mujibu wa Sheria za kazi ambapo Sheriaya Ajira (Employment Ordinance), Cap.366 ya 1957  jambo ambalo linavunja uwepo wa Sheria Na.82 ya mwaka 1962,iliyotungwa ili kuongeza marupurupu mbalimbaliYa mfanyakazi kama vile, mafao ya kuachishwa kazi, likizo na huku
Sheria ya kiinua mgongo “Severance Allowance Act” Na. 57 ya mwaka
1962,ikitoa haki na utaratibu wamalipo ya kujikimu baada ya kuachishwakazi.
Wafanyakazi hao pia wamelalamikia uvunjwajiwa Sheria Na.62 ya mwaka1964, Sheria ya Usalama Kazini(Security of Employment Act) kwa kufanyishwa kazi masaa mengi bila kupumzika jambo ambalo inasemekana kuwandiyo chanzo cha  Ajari Sheria hii ilianzishwa ilikupunguza uwezo wa waajiri kuajiri na kufukuza wafanyakazi na kuainisha aina za makosa na adhabu zake.

Rekebisho la Sheria Namba 17 la mwaka1983.lililenga kubadilisha
Viwango vya juu vya malipo kwa ulemavu wa kudumu na magonjwa
Yatokanayo na kazi kutoka shilingi 36,000/= hadi shilingi 108,000/= na
Kwa vifo kutoka shilingi 29,000/= hadi shilingi 83,000/=

Wakala wa Afyana Usalama Mahali pa kazi (OSHA) ulianzishwa kwa lengo la kusimamia masuala yote ya afya na usalama sehemu za kazi ili kupunguza ajari na magonjwa yatokanayo na kazi na hatimaye kuongeza tija.

Aidha kwa kupitia wakala wa Afya na Usalama Mahali pa kazi (OSHA) Wizara imefanikiwa kufanya kaguzi kama inavyoonyeshwa katika
Jedwali hapa chini

MWAKA
KUPIMA AFYA
KAGUZI ZA
KAWAIDA
KAGUZI
MAALUM
2001-2005

23,864
26,000
9,612
2006-2010
44,463
22,234
 50,979
JUMLA
68,327
31,846
76,979

Kutokana na kaguzi hizo, wakala umeweza kubaini baadhi ya waajiri ambao
Hawatoi taarifa za ajari zinapotokea na ambao hawasajili sehemu za kazi na
Kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kutozwa faini na wengine
Kupelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka kwa hatua zaidi.

Akizungumza na Tanzania daima Afisa mmoja wa Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa kazi Mkoani Mwanza ambaye hakutaka kuandikwa jina lake gazetini kwa sababu za kiusalama ameliambia Tanzania daima kuwa ni kweli upo uzembe uliobainika katika Kiwanda cha Sayona katika kipindi cha mwaka 2012 ambapo  Kiwanda cha Sayona kimetozwa faini mara mbili mfurulizo kutokana na uzembe na huduma duni katika masuala ya Usalama mahala pa kazi kwa wafanyakazi wake.

HAWA NDIYO MOJA WA MAJERUHI WA KIWANDA CHA SAYONA JIJINI MWANZA WAKIHANGAIKA NA VIDONDA
BAADA YA KULIPUKIWA NA JIKO LA KUYEYUSHIA VYUMA KATIKA KIWANDA CHA HICHO.



 Majeruhi wa Kiwanda cha Sayona LUCAS LUBINZA akiwa ameumia vibaya baada ya kulipukiwa na jiko la kuyeyushia vyuma katika kiwanda cha Sayona  kilichopo Nyang'homango Jijini Mwanza Picha na ANTONY SOLLO
 
 Majeruhi wa Kiwanda cha Sayona Lucas Nkalango akiwa ameumia vibaya baada ya kulipukiwa na jiko la kuyeyushia vyuma katika kiwanda cha Sayona  kilichopo Nyang'homango Jijini Mwanza Picha na ANTONY SOLLO



  Majeruhi wa Kiwanda cha Sayona LUCAS LUBINZA akiwa ameumia vibaya sehemu ya nyuma baada ya kulipukiwa na jiko la kuyeyushia vyuma katika kiwanda cha Sayona  kilichopo Nyang'homango Jijini Mwanza Picha na ANTONY SOLLO


 Kwa upande wa nyuma anavyoonekana Lubinza akiwa ameungua vibaya


Saturday, April 6, 2013

Abuse by Police and wife



Abuse by Police and wife






Inbox

x






Description: https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/profile_mask2.png
Present kalalu Kinyala <kinyalapresentkalalu@yahoo.com
11:49 am (1day ago)
Description: https://mail.google.com/mail/images/cleardot.gif

Description: https://mail.google.com/mail/images/cleardot.gif
Description: https://mail.google.com/mail/images/cleardot.gif
Description: https://mail.google.com/mail/images/cleardot.gif
  
Nimebahatika kwa jinsi ya bahati tuu kugundua uwepo wa chama kinachotetea wanaume wanaofanyiwa vitendo vya aibu na wake zao.

 Kwa bahati mbaya zaidi jamii yetu imekuwa na kawaida ya kuwasikiliza wanawake zaidi na kudhani ni wanyonge na hawawezi kufanya ukatili.

Ukatili niliofanyiwa ni kama ifuatavyo. Mwaka wa 2010 mwezi wa nane tarehe mbili askari wa kituo cha tumbi walikuja kwenye kituo cha Kobili Picha ya ndege pamoja na mke wangu wakakamata gari kubwa la biashara ambalo nilikua nimepaki hapo wakaondoka nalo wakidai lilikua gari la wizi.

 Nimekua nikiwadai Polisi hili gari tokea muda huo nimefuatilia hadi ngazi za juu za Polisi hakuna anayeweza kuniambia kwanini walishika gari langu. Nimewaandikia barua ya notice wamekaa kimya, Nimewaona ana kwa ana waishia kudai wanachunguza tukio.
Ni mwaka wa tatu sasa sina kazi sina jinsi ya kupata kipato nje ya hilo gari ambalo lilikuwa ni ajira yangu,Uchunguzi wangu umenipelekea kwenye ukweli kwamba nilifanyiwa kitendo cha ujambazi na Polisi.
Kuna jinsi wanashindwa kumchukulia hatua huyu Polisi aliyefanya huu ujambazi. Pengine kuna shinikizo kutoka nisipopajua. Kama kweli hili gari lilikua la wizi ni mwaka wa tatu sasa kwanini hawamtaki mwizi wampeleke kwenye vyombo vya sheria. 

Nina vielelezo vya kutosha nina omba msaada wenu.

 Ninaitwa Present Kalalu Kinyala


Description: https://mail.google.com/mail/images/cleardot.gifReply

Description: https://mail.google.com/mail/images/cleardot.gifForward




Hii imetumwa kwetu na mwenye Email iliyoko hapo juu tuifanyie kazi kama TAMRA